• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Muundo wa Taasisi

MUUNDO WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Tume inaundwa na Wajumbe saba (7), miongoni mwao wakiwemo Mwenyekiti na

Makamu Mwenyekiti ambao wanapaswa kuwa na sifa ya Jaji wa Mahakama Kuu au

Mahakama ya Rufani. Katika Uteuzi, Rais anazingatia kuwa endapo Mwenyekiti ni

mtu anayetoka sehemu moja ya Muungano, Makamu wake atakuwa ni mtu

anayetoka sehemu ya pili ya Muungano. Hii, ni kwa mujibu wa Ibara ya 74(1) na (2)

ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, na Kifungu cha

4(1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.


Aidha, Mjumbe mmoja anateuliwa kutoka miongoni mwa Wanachama wa Chama cha

Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society - TLS) na Wajumbe wengine

wanne (4) wanatakiwa wawe na uelewa wa kutosha kuhusiana na kusimamia na

kuendesha Uchaguzi wa Wabunge au sifa nyingine kama ambavyo Rais wa Jamhuri

ya Muungano atakavyoona inafaa kwa ajili ya kuendesha shughuli za Tume.

Tume ina jumla ya Wajumbe saba (7), kama inavyoonesha hapa chini:-


Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi

Na. Jina Wadhifa

1. Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele, Mwenyekiti

2. Mhe. Jaji Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk, Makamu Mweyekiti

3. Mhe. Jaji Asina Abdillah Omari, Mjumbe

4. Mhe. Jaji (Mst) Thomas Mihayo, Mjumbe

5. Mhe. Balozi Omar Ramadhani Mapuri, Mjumbe

6. Mhe. Magdalena Kamugisha Rwebangira, Mjumbe

7. Mhe. Jaji Rufaa Mwanaisha Athuman Kwariko, Mjumbe


Wajumbe wa Tume hukaa Madarakani kwa kipindi cha miaka mitano tangu

kuteuliwa kwao, lakini Rais anaweza kuwateua tena kwa kipindi kingine kadri

atakavyoona inafaa.

Katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume husaidiwa na Sekretarieti

inayoongozwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye ndiye Mtendaji Mkuu na Katibu

wa Tume. Kwa sasa Mkurugenzi wa Uchaguzi ni Ndugu Ramadhani Kombwey Kailima.


Aidha, Tume ina Idara 6, Ofisi ya Zanzibar na Vitengo 3 kama ifuatavyo:-


(i) Idara ya Usimamizi wa Uchaguzi;

Bofya Majukumu ya Idara ya Usimamizi wa Uchaguzi


(ii) Idara ya Daftari na TEHAMA;

Bofya Majukumu ya Idara ya Daftari na TEHAMA


(iii) Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura;

Bofya Majukumu ya Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura


(iv) Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu;

Bofya Majukumu ya Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu


(v) Idara ya Mipango Ufuatiliaji na Tathmini;

Bofya Majukumu ya Idara ya Mipango Ufuatiliaji na Tathmini


(vi) Idara ya Usimamizi wa Manunuzi na Lojistiki;

Bofya Majukumu ya Idara ya Usimamizi wa Manunuzi na Lojistiki


(vii) Ofisi ya Zanzibar;

Bofya Majukumu ya Ofisi ya Zanzibar


(viii) Kitengo cha Huduma za Sheria;

Bofya Majukumu ya Kitengo cha Huduma za Sheria


(ix) Kitengo cha Fedha na Uhasibu; na

Bofya Majukumu ya Kitengo cha Fedha na Uhasibu; na


(x) Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani;

Bofya Majukumu ya Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani

Habari Mpya

  • Tume yatwaa Kombe Mchezo wa Kuvuta Kamba kwenye Bonanza la Ukaguzi
    March 20, 2023
  • Tume yashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar
    January 02, 2023
  • Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa kushiriki Uchaguzi Mdogo Jimbo la Amani na Kata Saba
    December 16, 2022

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Mpango Mkakati wa NEC 2021/22 – 2025/26
  • Taarifa ya Tathmini ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2020
  • Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa mwaka 2020
  • Wabunge Wanawake Walioteuliwa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi