Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imewataka Wasimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo la Ushetu katika Halmashauri ya Ushetu Mkoani Shinyanga na Kata 10 za Tanzania bara kutokufanya kazi ya Uchaguzi kwa mazoea na badala yake wazingatie maelekezo, kanuni na sharia za uchaguzi katika utendaji wao.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza Uchaguzi Mdogo wa Udiwani katika Kata Sita za Tanzania Bara utakaofanyika tarehe 9 Oktoba mwaka 2021.
?TUME ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza kuwepo kwa nafasi mbili za Ubunge katika majimbo ya Konde mkoa wa Kaskazini Pemba na Ushetu mkoani Shinyanga.
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Konde na Udiwani katika Kata Sita za Tanzania Bara utakaofanyika tarehe 18 Julai mwaka 2021.
?Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buhigwe Felix Kavejuru amepata ushindi katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo baada ya kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine.
Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Muhambwe Dkt. Florence Samizi amepata ushindi katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo baada ya kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine.