Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imesisitiza kuwa Watanzania wanaokwenda kuandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wawe na nanmba za simu za mkononi kwani mashine ya BVR hairuhusu kumuandisha mwananchi bila kuweka namba ya simu.
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Mbarouk Salum Mbarouk amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa wazee wa kimila Mkoani Manyara ili kufanikisha Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mkoa huo.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Semistocles Kaijage amesema Tume haijaagiza wapiga kura walipoteza kadi zao za kupigia kura kudaiwa taarifa ya upotevu (loss report) ili wapatiwe kadi mpya.
Wito umetolewa kwa Wanawake kujitokeza kwa wingi wakati wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili kujiandikisha na kuboresha taarifa zao na hatimaye waweze kushiriki katika Uchaguzi Mkuu ujao wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2020.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Singida Mashariki utakaofanyika tarehe 31 Julai mwaka huu
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewataka viongozi wa dini kuwahimiza waumini wao juu ya kushiriki kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura au kuboresha taarifa zao ili kila mwananchi mwenye sifa za kuandkishwa akaandikishwe na yule anayeboresha taarifa zake akaboreshe.