Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imemtangaza Dkt. John Pombe Joseph Magufuli mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu wa Rais katika Uchaguzi wa Rais uliofanyika tarehe 28 Oktoba, 2020.
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeongeza siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi katika majimbo yote nchini kuapisha mawakala wa vyama vya saisa kwa ajili ya siku ya uchaguzi tarehe 28 Oktoba, 2020.
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi imefanya uamuzi wa rufaa 616 za wagombea ubunge na udiwani katika Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Oktoba 28, 2020.
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi imezipitia, imechambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 87za wagombea udiwani na kuwarejesha wagombea 47 wa udiwani na kuwarejesha wagombea udiwani katika orodha ya wagombea udiwani.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imezipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 50 za wagombea ubunge na udiwani ambapo kati ya rufaa hizo 4 ni za wagombea ubunge na 46 ni za wagombea udiwani.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imezipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 46 za wagombea udiwani waliowasilisha rufaa zao Tume kutoka kata mbalimbali nchini.