Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
?TUME ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza kuwepo kwa nafasi mbili za Ubunge katika majimbo ya Konde mkoa wa Kaskazini Pemba na Ushetu mkoani Shinyanga.
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Konde na Udiwani katika Kata Sita za Tanzania Bara utakaofanyika tarehe 18 Julai mwaka 2021.
?Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buhigwe Felix Kavejuru amepata ushindi katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo baada ya kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine.
Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Muhambwe Dkt. Florence Samizi amepata ushindi katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo baada ya kupata kura nyingi zaidi ya wagombea wengine.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewataka mawakala wa vyama vya siasa na wasimamizi wa uchaguzi kuzingatia Sheria za Uchaguzi wakati wote wanapotekeleza majukumu yao katika Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika majimbo ya Muhambwe na Buhigwe mkoani Kigoma na Uchaguzi wa Udiwani katika kata tano za Tanzania Bara
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeshiriki kwenye Mkutano wa Kamati Tendaji (Exucutive Committee) ya Jukwaa la Jumuiya ya Tume za Uchaguzi kutoka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (ECF SADC) wenye lengo la kuimarisha usimamizi wa uchaguzi na kukuza demokrasia nchi.