Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wanahudhuria mafunzo ya siku tano (5) ya Uongozi wa kimkakati yanayofanyika katika Ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani amesema jambo kubwa ambalo watanzania wanapaswa kujifunza kutokana na Uchaguzi wa Marekani uliomalizika hivi karibuni ni kwa wananchi kuheshimi mifumo ya Uchaguzi.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani ameunga na familia ya marehemu kuomboleza msiba wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri, marehemu Samuel Sitta nyumbani kwake jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Damian Lubuva amewasihi viongozi na wafanyakazi wa Tume hiyo kuzingatia nidhamu ya kazi ili kuleta ufanisi katika kutekeleza majukumu yao.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) itazialika Asasi za Kiraia zinazotaka kutoa Elimu ya Mpiga Kura kutuma maombi ya kupata kibali cha kutoa Elimu hiyo ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata Elimu ya Mpiga Kura.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekabidhi Taarifa ya Tathmini baada ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2015 kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu , Sera, Bunge, Kazi , Ajira, Vijana na Walemavu Mh. Jenista Mhagama mjini Dodoma leo.