Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa kura zinazoharibika kwenye chaguzi zinasababishwa na wapiga kura kukosa elimu ya mpiga kura.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa wito kwa wananchi walioko kwenye halmashauri mbalimbali nchini, kuitumia vyema fursa ya utoaji wa elimu ya mpiga kura kupitia redio za kijamii kwenye halmashauri zao ili kuondoa manung’uniko kwenye chaguzi.
Watumishi Tume ya Taifa ya Uchaguzi waadhimisha Sherehe za Meimosi mwaka 2017 jijini Dar es salaam.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza kuwepo kwa nafasi wazi ya Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA, kufuatia kifo cha Mbunge wa Viti Maalum wa chama hicho Mhe. Dr. Elly Marko Macha aliyefariki tarehe 31 Machi 2017.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Mhe. Jaji (R) Semistocles Kaijage amewataka watumishi wa tume hiyo wazingatie maadili na kanuni za utawala bora ili kutekeleza kwa ufanisi jukumu la Tume katika kukuza na kuimarisha demkorasi na utawala bora nchini.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewatahadharisha watu wanaochukua kadi za kupigia kura za wenzao na kuzizuilia au kubaki nazo kuwa ni kinyume cha Sheria.