Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeendelea na utaratibu wa kutoa elimu ya mpiga kura kila wakati kuhakikisha kuwa Watanzania wanakuwa na uelewa mpana kuhusu masuala ya uchaguzi nahatimaye waweze kujitokeza kwa wingi katika kupiga kura.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imemteua Ndugu Rehema Juma Migilla kuwa Mbunge wa Viti Maalum katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Wananchi (CUF) ,kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Ndugu Hindu Hamisi Mwenda aliyefariki dunia Septemba 1, 2017.
MKURUGENZI wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhan amevitaka vyombo vya Habari vya Tanzania viige mfano wa wenzao wa Kenya kwa kutumia muda mwingi kutoa Elimu ya Moiga kura.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kuendelea kusimamia matumizi bora ya rasilimali inazopewa na Serikali na kuzitaka taasisi nyingine za Serikali kuiga mfano huo.
Katika Maoni ya Mhariri ya Gazeti la MwanaHalisi Toleo Na. 402 la Jumatatu, tarehe 31 Julai – 06 Agosti, 2017, yenye kichwa cha habari “Kwa hili, NEC imechafuka zaidi”.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeanza maandalizi ya kufanya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 baada ya Serikali kutenga Shilingi Bilioni 10 kwa ajili ya kazi hiyo katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha.