• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Watumishi wa Tume wachangia damu, wafanya usafi Kituo cha Afya Makole kuadhimisha Wiki ya Utumishi

Imewekwa: June 22, 2023

Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) leo tarehe 22 Juni, 2023, wamechangia chupa 14 za damu na kufanya usafi wa mazingira katika kituo cha Afya Makole kilichopo jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 16-23 juni.

Watumishi hao wakiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Raslimali Watu Bw. Leonard Tumua kwanza walifanya usafi wa mazingira kwa kufyeka majani na kukusanya takataka katika maeneo mbalimbali ya kituo hicho, na kufuatiwa na zoezi la kutoa damu.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa zoezi la kutoa damu, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makole Dkt.Revocatus Bartazar amewashukuru watumishi hao kwa kuchangia kiasi hicho cha damu kwani mahitaji ya damu katika kituo hicho kwa akina mama wanaojifungua ni makubwa.

Amesema kwa mwezi akina mama 600 hadi 700 hujifungua katika kituo hicho na mahitaji ya damu ni makubwa kwani asilimia 10 ya akina mama wanaojifungua hukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Amesema sababu kubwa inayopelekea akina mama wanaojifungua kupoteza maisha ni kupoteza damu nyingi baada ya kujifungua.

“Sababu kubwa inayopelekea vifo vya akina mama wanaojifungua nchini Tanzania ni kutoka damu nyingi baada ya kujifungua,” amesema Dkt Bartazar.

Ameongeza kuwa zaidi ya asilimia 90 ya vifo vitokanavyo na uzazi vinatokana na damu kutoka nyingi baada ya kujifungua hivyo njia ya kupunguza vifo vya aina hiyo ni kwa wananchi kujitokeza kuchangia damu kama walivyofanya watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Amesema mama aliyepoteza damu nyingi kutokana na kujifungua akipata chupa moja inamsaidia kuweza kurudisha uhai wake, hivyo kwa watumishi hao kuchangia chupa 14 wameweza kuokoa uhai wa akina mama 14 watakaohitaji damu .

Naye Mratibu wa Kitengo cha Damu Salama wa Kituo hicho cha Afya Bw.Jerome Felician Marando amewapongeza watumishi wa NEC kwa kuchangia chupa 14 za damu kwani amesema kiasi hicho ni kikubwa kwani mara nyingi wanapofanya mazoezi ya kuhamasisha watu kuchangia damu wanapata chupa 5 au 6 hivyo kupata chupa 14 ni kitu kikubwa sana kwa mahitaji ya Kituo cha Afya Makole.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Utawala na Raslimali Watu Bi. Felister Ishuza amesema shughuli ya usafi na kuchangia damu iliyofanywa na watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilikuwa ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 16-23 juni.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi