• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Watendaji wa Uchaguzi Jimbo la Amani Zanzibar watakiwa kuzingatia katiba, sheria za uchaguzi

Imewekwa: November 16, 2022

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewataka watendaji wa uchaguzi katika Jimbo la Amini Tanzania Zanzibar kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano, sheria za uchaguzi na kanuni zake, Maadili ya Uchaguzi na maelekezo ya Tume.

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Tume Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri wakati akifungua mafunzo kwa wasiamamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi katika Jimbo la Amani yaliyofanyika tarehe 16 Novemba 2022, kwenye Ofisi za Tume zilizopo Unguja.

Alisema sanjari na kuzingatia miongozo hiyo, Mhe. Balozi Mapuri aliwaasa watendaji hao wa uchaguzi kuvishirikisha vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi katika jimbo hilo ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao ya uchaguzi.

Aliongeza kuwa uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbalimbali za kufuatwa na kuzingatiwa kwani hatua na taratibu hizo ndiyo msingi wa uchaguzi mzuri, wenye ufanisi na unaopunguza malalamiko na vurugu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.

“Ni muhimu kwenu pia kuhakikisha mnayatambua na kuyajua vyema maeneo ambayo chaguzi zitandeshwa ikiwemo miundombinu ya kufika katika kata na vituo vya kupigia kura” alisema Balozi Mapuri nakuongeza kuwa:

“Pamoja na mambo niliyoyaanisha hapo awali, napenda kuwasisitiza kufanya utambuzi wa vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo husika kwa lengola kuhakikisha mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani”

Aliwataka watendaji hao kuhakikisha wanawaajiri watendaji wa vituo wenye weledi, wanaojitambua na kwa kadri inavyowezekana waachane na undugu au upendeleo kwa ndugu na jamaa wasio na sifa za kufanya shughuli za uchaguzi.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilitangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Amani Tanzania Zanzibar na Udiwani katika kata 12 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika tarehe 17 Desemba mwaka 2022.

Habari Mpya

  • Tume yatwaa Kombe Mchezo wa Kuvuta Kamba kwenye Bonanza la Ukaguzi
    March 20, 2023
  • Tume yashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar
    January 02, 2023
  • Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa kushiriki Uchaguzi Mdogo Jimbo la Amani na Kata Saba
    December 16, 2022

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Mpango Mkakati wa NEC 2021/22 – 2025/26
  • Taarifa ya Tathmini ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2020
  • Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa mwaka 2020
  • Wabunge Wanawake Walioteuliwa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi