• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Wadau wa Uchaguzi watakiwa kuwahamasisha wanachi kata ya ikoma wilayani Rorya kushiriki uboreshaji

Imewekwa: November 20, 2023

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewataka wadau wa uchaguzi kufikisha ujumbe sahihi kwa wananchi wa Kata ya Ikoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ili wananchi wenye sifa ya kuandikishwa na kuboresha taarifa zao wajitokeze kwa wingi kushiriki uboreshaji wa majaribio wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuwabainisha waliopoteza sifa za kuwa wapiga kura.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Ramadhani Kailima wakati akifungua mkutano wa Tume na wadau wa uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Mapsap Linme iliyopo wilayani Rorya Mkoa wa Mara.

Aliwaasa wadau wote wa uchaguzi kuendelea kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo katika kipindi chote cha uboreshaji wa majaribio wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

“Ni tegemeo la Tume kuona mnafikisha ujumbe sahihi kwa wananchi ambako uboreshaji wa majaribio yatafanyika ili wananchi wenye sifa ya kuandikishwa na kuboresha taarifa zao wajitokeze kwa wingi kushiriki zoezi hili na kuwabainisha waliopoteza sifa za kuwa wapiga kura.

Pia, nawaasa wadau wote kuendelea kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo katika kipindi chote cha uboreshaji wa majaribio la Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.”, alisema Bw. Kailima.

Mbali na kuwaasa wadau hao wa uchaguzi, Mkurugenzi wa Uchaguzi alisema kuwa Tume imejipanga kuhakikisha kuwa wananchi wanapata uelewa wa kutosha kuhusu uboreshaji wa majaribio kwa kutumia njia mbalimbali za kutoa elimu ya mpiga kura zikiwemo; kukutana na wadau wengine wa uchaguzi.

Aliongeza kuwa vyama vya siasa vitashiriki katika uboreshaji wa majariobio kwa kuweka wakala mmoja katika kila kituo cha kuandikisha wapiga kura, lengo ni kushuhudia na kujiridhisha juu ya taratibu zitakazotumika wakati wa uboreshaji wa majaribio wa Daftari.

Alisisiti kwa kuwaomba wadau wa uchaguzi kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni na mapendekezo kwenye mkutano huo ili kufanikisha utekelezaji wa uboreshaji huo.

Mkutano huo wa wadau wa uchaguzi umewashirikisha viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, wazee wa kimila, watu wenye ulemavu, wawakilisha wa vijana, wawakilishi wa wanawake na asasi za kiraia kwa ujumla kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi itafanya uboreshaji wa majaribio wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Kata ya Ikoma iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Mkoa huu wa Mara na Kata ya Ng’ambo iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, mkoa wa Tabora, utakaofanyika kuanzia tarehe 24 hadi 30 Novemba, 2023.

Habari Mpya

  • Wadau wa Uchaguzi watakiwa kuwahamasisha wanachi kata ya ikoma wilayani Rorya kushiriki uboreshaji
    November 20, 2023
  • Tume yatangaza kuanza Uboreshaji wa Majaribio
    November 10, 2023
  • Tume yafanya Uteuzi wa Mbunge wa Viti Maalum
    November 03, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi