• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Vyama vitano vyachukua fomu za uteuzi Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali

Imewekwa: August 14, 2023

Vyama vitano vya Siasa vimechukua fomu za uteuzi wa wagombea Ubunge katika Jimbo la Mbarali Mkoa wa Mbeya kuwania kiti hicho katika Uchaguzi Mdogo wa Ubunge unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 Septemba mwaka 2023.

Vyama vilivyochukua fomu ni Chama cha AAFP kikiwakilishwa na Bi. Halima Abdalah Magomba, Chama cha DP kupitia kwa Bw. Osward Joseph Mndeva, Chama cha UDP kikiwakilishwa na Bw. Zavely Laurent Seleleka, Chama cha CCK kilichomtea Bw. Exavery Town Mwataga kuwa mgombea wake na Chama cha UPDP kikiwalishwa na Bw. Bosco Daudi Mahenge.

Wagombea wa vyama hivyo wamekabidhiwa fomu za uteuzi na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mbarali Bw. Missama Kwangura katika Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali.

Akizungumza wakati wa kukabidhi fomu hizo, Bw. Kwangura aliwakumbusha wagombea wa vyama hivyo kujaza fumo hizo kwa usahihi ikiwemo wadhamini wasiopungua 25 walioandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la Jimbo la Mbarali.

“Kwa kuzingatia taratibu za uteuzi baada ya kujaza fomu hizi mnaweza kuzileta siku tatu kabla ya siku ya uteuzi ili tuweze kuzihakiki na kufanya marekebisho pale ambako kuna mapungufu katika kujaza fomu hizi” alisema Bw. Kwangura.

Aliwapongeza wagombea hao kwa kuonesha nia ya kugombea kiti cha Ubunge katika jimbo hilo kwani hatua hiyo inaimarisha demikrasia katika uchaguzi nchini.

Utoaji fomu za uteuzi kwa wagombea umeanza jana tarehe 13 hadi 19 Agosti, 2023 ambayo itakua siku ya uteuzi wa wagombea katika Uchaguzi Mdogo wa Ubunge Jimbo la Mbarali na Udiwani katika Kata Sita za Tanzania Bara.

Kwa mujibu wa ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kampeni za uchaguzi zitaanza tarehe 20 Agosti hadi tarehe 18 Septemba na tarehe 19 Septemba, 2023 itakuwa siku ya kupiga kura.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi