• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume yawataka wasimamizi wa uchaguzi kuvishirikisha vyama vya siasa wakati wa uchaguzi

Imewekwa: June 19, 2023

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewataka Masimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo na Kata kuvishirikisha vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi katika masuala ya kiuchaguzi ambayo wanastahili kushirikishwa ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao.

Hayo yamesema na Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Thomas Mihayo wakati akifungua mafunzo kwa wasimamizi hao wa uchaguzi yanayofanyika Mjini Iringa, ikiwa ni maandalizi ya Uchaguzi Mdogo wa Madiwani katika kata 14 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika tarehe 13 Julai mwaka 2023.

Alisema iwapo kuna mambo hayahitaji kuwashirikisha wadau hao wasiwashirikishe na wala wasishinikizwe kuwashirikisha na kama yapo mambo ambayo wanapaswa kuwashirikisha basi ni lazima wawashirikishe ili kurahisisha majukumu yao.

Jaji Mst. Mihayo aliongeza kwa kuwataka wasimamizi hao wa uchaguzi kufuata na kuzingatia hatua na taratibu za kisheria katika kutekeleza majukumu yao kwani hatua na taratibu hizo ndio msingi wa uchaguzi kuwa mzuri na wenye ufanisi na hupunguza malalamiko katika uchaguzi.

“Uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbalimbali za kisheria ambazo hupaswa kufuatwa na kuzingatiwa kwani hatua na taratibu hizo ndio msingi wa uchaguzi kuwa mzuri, wenye ufanisi na hivyo kupunguza kama si kuondoa malalamiko au vurugu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi”, alisema Jaji Mst. Mihayo na kuongeza:

“Jambo muhimu mnalotakiwa kuzingatia ni kujiamini na kufanya kazi kwa weledi na kwamba katika utendaji wa majukumu yenu, mnapaswa kuzingatia Katiba ya nchi, sheria za uchaguzi na kanuni zake, Maadili ya Uchaguzi na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na yatakayotolewa na Tume katika kipindi hiki cha uchaguzi mdogo”.

Aliwasisitiza wasimamizi hao wa uchaguzi kuzingatia masuala muhimu ikiwa ni pamoja na kufanya utambuzi wa vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo husika kwa lengo la kuhakikisha mpangilio mzuri unaoruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani.

Jaji Mst. Mihayo aliwataka wasimamizi hao kuhakikisha wanaajiri watendaji wa vituo wenye weledi, wanaojitambua na kwa kadri inavyowezekana waachane na upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya shughuli za uchaguzi.

“Kuhakikisha vifaa vya uchaguzi mnavyovipokea kutoka Tume na kuhakikisha kila mkuu wa kituo anapata vifaa vyote vya uchaguzi vinavyohitajika mapema. Kuhakikisha siku ya uchaguzi mnaweka utaratibu utakaowezesha kila kituo cha kupigia kura kinafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufanya mawasiliano na Tume pale ambapo utahitajika ushauri kuhusiana na masuala ya uchaguzi uliopo.”, alisema Jaji Mst. Mihayo.

Mafunzo haya ya siku tatu kwa Masimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi lengo lake ni kuwajengea uwezo na kuwakumbusha wajibu na majukumu yao wakati wote wa uchaguzi na yanafanyika pia katika mkoa wa Tanga kwa watendaji wengine wanaotarajia kusimamia uchaguzi mdogo kutoka katika halmashauri nyingine.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi