• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa Tume kwa mwaka 2016/2017 hadi 2020/2021
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Tume yatoa uamuzi wa rufaa 60 za wagombea ubunge na udiwani na kuwarejesha wagombea 34 wa udiwani kwenye uchaguzi

Imewekwa: September 11, 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imezipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 60 kati ya hizo rufaa 2 ni za wagombea ubunge na 58 ni za wagombea udiwani katika kikao chake cha jana tarehe 10 Septemba 2020.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam leo tarehe 11 Septemba, 2020 na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Wilson Mahera Charles kufuatia kukamilika kwa uamuzi dhidi ya rufaa hizo.

Dkt. Charles amesema Tume katika rufaa hizo imekubali rufaa moja na kumrejesha mgombea katika orodha ya wagombea kutoka kwenye Jimbo la Iramba Magharibi na kukataa rufaa moja ya mgombea ambaye uteuzi wake ulitenguliwa kutoka kwenye Jimbo la Iramba Magharibi.

Amesema Tume imezipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 58 za madiwani na kukubali rufaa 34 na kuwarejesha wagombea katika orodha ya wagombea udiwani.

Amezitaja kata ambazo wagombea wake wamerejeshwa kuwa ni Kata za Kahororo (Bukoba), Ishozi (Nkenge),Chongoleani (Tanga Jiji), Kirare (Tanga Jiji), Mwamanga (Magu), Ng’haya (Magu), Riroda (Babati Vijini), Maswa Magharibi (Maswa), Kirumba (Ilemela), na kata ya Bonga (Babati Vijini).

Kata nyingine ni Kamagambo (Karagwe), Namelock (Kiteto), Masewa (Bariadi), Bweranyange (Karagwe), Kituntu (Karagwe), Kamagambo (Karagwe), Msowero (Kilosa), Lubugu (Magu), Lingeta (Meatu), Ifakara (Kilombero), Kiloli (Sikonge), Mkoma (Rorya), na kata ya Nyamhongolo (Ilemela)

Dkt. Charles amezitaja kata nyingine kuwa ni kata ya Sikonge (Sikonge), Tanganyika (Muheza), Uhenga (Wanging’ombe), Babati (Babati), Vwawa (Mbozi), Lukanga (Mkuranga), Langai (Simanjiro), Lutale (Magu), Majohe (Ilala), Namabengo (Namtumbo) na Viwanja Sitini (Kilombero).

Katika hatua nyingine, Dkt. Charles amesema pia Tume imekataa rufaa 23 za wagombea ambao hawakuteuliwa kutoka kwenye Kata za Ilemela (Ilemela), Kayenze (Mwanza Jiji), Kiarare (Tanga Jiji), Mabawa (Tanga Jiji), Ilemela (Ilemela), Kadoto (Maswa Magharibi), na kata ya Iyela (Mbeya Jiji).

Kata nyingine ambazo wagombea wake rufaa zao zimekataliwa ni kata ya Kirua Vunjo Magharibi (Vunjo), Mji Mpya (Morogoro Mjini), Pugu (Ukonga), Tembela (Mbeya Mji), Vikumburu (Kisarawe), Mecco (Ilemela), Kibara (Mwibara), Kiloleli (Sikonge), Changarawe (Mafinga Mji), Igawilo (Mbeya Mjini), Msonga (Mkuranga), Uru Kaskazini (Moshi Vijini), Kivukoni (Ilala), Maanga (Mbeya Mjini), Nsalaga (Mbeya Mjini) na Jangwani (Ilala).

“Tume pia imekataa rufaa 1 ya kupinga walioteuliwa. Rufaa hiyo ni kutoka kwenye Kata ya Arri (Babati Vijijini).Idadi hii inafanya jumla ya rufaa za wagombea Ubunge zilizofanyiwa uamuzi na Tume kufikia 113 na za wagombea Udiwani 103”, amesema Dkt. Charles.

Amesema Tume itaendelea kutoa matokeo baada ya usajili na uchambuzi wa rufaa hizo kila siku na kwamba wahusika wa rufaa hizo watajulishwa kwa barua juu ya uamuzi wa Tume.

Habari Mpya

  • Tume yashiriki mkutano wa ECF SADC kuimarisha usimamizi wa uchaguzi na kujenga demokrasia nchini
    March 11, 2021
  • Tume yamtangaza Dkt. Magufuli kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Oktoba 28, 2020
    October 31, 2020
  • Tume yaongeza siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuapisha mawakala wa vyama vya siasa kwa ajili ya uchaguzi
    October 23, 2020

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Orodha ya Madiwani Wateule wa Viti Maalum walioteuliwa na Tume katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
  • Orodha ya Madiwani Wateule wa Viti Maalum wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2020
  • Orodha ya Wagombea wa Kiti cha Rais
  • Orodha ya Wagombea Ubunge
  • Wagombea waliopita bila kupingwa

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, Uchaguzi House, Njedengwa Investment Area, Block D, Plot No. 4
  • Namba ya Simu : +255 22 2114963-6
  • Nukushi : +255 22 2116740, +255 22 2127075
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2021 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi