• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa Tume kwa mwaka 2016/2017 hadi 2020/2021
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Tume yatoa uamuzi wa rufaa 46 za wagombea udiwani na kuwarejesha wagombea 24 kwenye uchaguzi

Imewekwa: September 12, 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imezipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 46 za wagombea udiwani waliowasilisha rufaa zao Tume kutoka kata mbalimbali nchini.

Akitoa taarifa kwa umma jijini Dar es Salaam leo tarehe 12 Septemba, 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Dkt. Wilson Mahera Charles amesema kati ya rufaa hizo Tume imekubali rufaa 24 na kuwarejesha wagombea katika orodha ya wagombea Udiwani.

Ametaja kata ambazo wagombea wake wamerejeshwa kuwa ni kata ya Dunda (Bagamoyo), Mtwivila (Iringa Mjini), Kikilo (Kondoa), Makurumla (Ubungo), Hezya (Vwawa), Makorongoni (Iringa Mjini), Bwawani (Arumeru Magharibi), Jinjimili (Magu), Kimnyaki (Arumeru Magharibi).

Dkt. Charles ametaja kata nyingine kuwa ni kata ya Lemanyata (Arumeru Magharibi), Mkwawa (Iringa Mjini), Kisarawe II (Kigamboni), Makurumla (Ubungo), Mbabala (Dodoma Mjini), Mpanda Hotel (Mpanda Mjini), Lusungo (Kyela), Same (Same), Maisaka (Babati Mjini), Makuburi (Ubungo), Kibada (Kigamboni), Maore (Same Mjini) na rufaa tatu kutoka Kata ya Mshindo (Iringa Mjini).

Katika hatua nyingine, Dkt. Charles amesema Tume imekataa rufaa 13 za wagombea ambao hawakuteuliwa kutoka kwenye Kata za Kawajense (Mpanda), Mjini Chirombola (Ulanga), Mabokweni (Tanga Mjini).

Amezitaja kata nyingine kuwa ni Chanika (Karagwe), Mwamala (Manonga), Kiomboi (Iramba Magharibi), Mwasenkwa (Mbeya Mjini), Old Iramba (Iramba Magharibi), Magara (Babati Vijijini), Arri (Babati Vijijini), Chapwa (Tunduma) na rufaa mbili kutoka Kata ya Kibamba (Kibamba).

“Tume imekataa rufaa 9 za kupinga walioteuliwa kutoka kwenye Kata za Nonde (Mbeya Mjini), Mwagata (Iringa Mjini), Mabibo (Ubungo), Mkimbizi (Iringa Mjini), Kipanga (Sikonge), Nsoho (Mbeya Mjini), Ilemi (Mbeya Mjini), Bagara (Babati Vijijini) na Nkinga (Manonga)”, amesema Dkt. Charles.

Amesema idadi hiyo ya rufaa 46 inafanya jumla ya rufaa za wagombea Ubunge zilizofanyiwa uamuzi na Tume kufikia 113 na za wagombea Udiwani 149.

Tume itaendelea kutoa matokeo baada ya usajili na uchambuzi wa rufaa hizo kila siku na kwamba wahusika wa rufaa hizo watajulishwa kwa barua juu ya uamuzi wa Tume.

Habari Mpya

  • Tume yashiriki mkutano wa ECF SADC kuimarisha usimamizi wa uchaguzi na kujenga demokrasia nchini
    March 11, 2021
  • Tume yamtangaza Dkt. Magufuli kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Oktoba 28, 2020
    October 31, 2020
  • Tume yaongeza siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuapisha mawakala wa vyama vya siasa kwa ajili ya uchaguzi
    October 23, 2020

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Orodha ya Madiwani Wateule wa Viti Maalum walioteuliwa na Tume katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
  • Orodha ya Madiwani Wateule wa Viti Maalum wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2020
  • Orodha ya Wagombea wa Kiti cha Rais
  • Orodha ya Wagombea Ubunge
  • Wagombea waliopita bila kupingwa

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, Uchaguzi House, Njedengwa Investment Area, Block D, Plot No. 4
  • Namba ya Simu : +255 22 2114963-6
  • Nukushi : +255 22 2116740, +255 22 2127075
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2021 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi