• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume yakutana na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar

Imewekwa: December 14, 2017

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, amesema kuna amani na utulivu wa kutosha kwa Wananchi wa Zanzibar hasa baada ya kukamilika kwa Uchaguzi wa marejeo Visiwani humo uliofanyika Machi 20,2016.

Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar ulilazimika kurejewa baada ya kufutwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa awali uliofanyika Oktoba 25,2015,kutokana na kukiukwa kwa taratibu mbalimbali zinazosimamia na kuendesha uchaguzi na hivyo Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kulazimika kufuta matokeo ya Uchaguzi huo.

Makamu wa Pili wa Rais amesema hayo wakati akipokea taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani uliofanyika Oktoba 25,2015 toka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva,Ofisini kwake Vuga,Zanzibar leo.

Katika hotuba yake Makamu wa Pili wa Rais aliwaeleza Makamishna wa Tume kuwa, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilijitahidi kufanya mazungumzo na upande wa upinzani kupata muafaka kuhusina na kukiukwa kwa taratibu za Uchaguzi na nini kifanyike baada ya hapo.

Hata hivyo,tofauti na makubaliano ya mazungumzo,Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF),aliamua kufanya Mkutano na Waandishi wa habari baada ya vikao nane na hivyo kukiuka taratibu za kuendesha mazungumzo ya vikao hivyo.

Baada ya kukiukwa kwa taratibu hizo,serikali ilitangaza tarehe ya kurudiwa, kwa uchaguzi na vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi wa Oktoba 25,2015 walipaswa pia kushiriki katika uchaguzi wa marejeo ambapo chama cha Wananchi (CUF) ,hakikushiriki katika Uchaguzi huo.

Awali kabla ya kukabidhi taarifa hiyo,Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damiani Lubuva alimweleza Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd kuwa inaweza kuendelea mchakato wa majukumu mengine ikiwemo maandalizi ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Wakati huohuo,Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva alikabidhi taarifa hiyo ya Uchaguzi Mkuu kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi Zuber Ali Maulid katika ofisi za Bazara za Baraza hilo.

Katika hafla hiyo,Mwenyekiti alimweleza Spika wa Baraza la Wawakilishi kuwa ni muhimu kuimarisha uhusiano uliopo na kujenga ushirikiano zaidi ili kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kila siku.

Kwa upande wake, Spika Ali alisema amefurahishwa na ziara hiyo ya Makamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwani inatoa nafasi ya kuelewa jinsi ambavyo Baraza la Wawakilishi linatekeleza majukumu yake katika kuwahudumia wananchi waliowachagua.

Aidha,Mkurugenzi wa uchaguzi Bwana Kailima Ramadhani pia, alipata fursa ya kukabidhi taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar(ZEC) Bwana Salum Kassim Ali.

Katika ziara hiyo ya siku tatu ambayo ilikuwa ya kawaida,Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damin Lubuva alifuatana na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Hamid M. Hamid,Wajumbe wa Tume Jaji Mstaafu John Mkwawa na Mary H.C.S Longway,Mchanga H.Mjaka,Asina Omari na Katibu wa Tume na Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani.

Ziara hiyo imekamilika leo, na Wajumbe hao wa Tume wanajiandaa kwa ziara kama hiyo ambayo itafanyika mjini Dodoma kuanzia kesho tarehe 28/06/2016.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi