• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume yakagua eneo la ujenzi wa jengo la Ofisi Dodoma

Imewekwa: December 14, 2017

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damin Lubuva amesema Tume imeridhika na kufurahishwa na kiwanja ambacho imepatiwa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA),na Tume iko tayari kuanza taratibu za ujenzi katika eneo hilo.

Kiwanja hicho chenye ukubwa wa mita za eneo 36,000 sawa na ekari 10, kimeigharimu Tume ya Taifa ya Uchaguzi shilingi milioni 475 na kiko katika eneo la Ndenjengwa nje kidogo ya Manisapaa ya Dodoma.

Akizungumza na Waandishi wa Habari muda mfupi baada ya kutembelea eneo hilo, Jaji Lubuva amesema kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi inajivuna kupata eneo hilo na iko tayari kuanza ujenzi pindi taratibu zitakapokamilika na kuwa miongoni mwa Taasisi za Serikali ambazo zitahamia Dodoma.

Naye Mkurugenzi wa UIchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bwana Kailima Ramadhani, akizungumza katika hafla hiyo amesema kuwa,ufanisi katika utendaji wa Shughuli za Tume utaimarika baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Jengo la Tume kutokana na ukweli kuwa utekelezaji wa majukumu ufanyika katika jengo moja.

Kwa sasa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inatumia majengo ambayo yako sehemu tatu tofauti na kusababisha utendaji kuwa katika mazingira magumu ya utekelezaji wa majukumu. 2 Aidha,bwana Ramadhani amesema baada ya kukamilika kwa ujenzi wa jengo,watumishi watafanya kazi katika mazingira salama na tulivu ikilinganishwa na sasa ambapo Tume inatumia ofisi za kupanga ambazo pia zinatumiwa na wapangaji wengine.

Bwana Ramadhani amebainisha pia kuwa taratibu za maandalizi ya ujenzi wa jengo ziko mbioni ikiwemo kuandaa michoro ya jengo na kukamilisha taratibu nyingine za kuwapata wazabuni kwa ajili ya kufanya kazi ya ujenzi.

Kwa upande wake,Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA),Bwana Elius Mwakalinga amesema TBA iko tayari kutoa ushauri wa kujenga jengo bora pindi taratibu za michoro zitakapokamilika.

Bwana Mwakalinga amesema TBA iko tayari kushirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili kuhakikisha kuwa ujenzi wa jengo hilo unafanyika kwa kuzingatia taratibu na kuzingatia teknolojia ya kisasa kulinga na eneo ambalo jengo hilo litajengwa ili kukidhi mahitaji.

Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,wako katika ziara ya siku nne Mkoani Dodoma ambapo pamoja na kutembelea eneo la Kiwanja kwa ajili ya Ujenzi wa Ofisi za Tume,kesho 30/06/2016 wanatarajiwa kutembelea Ofisi za Bunge na Kuonana na Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi