• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa Tume kwa mwaka 2016/2017 hadi 2020/2021
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Tume yafanya uamuzi wa rufaa 50 za wagombea ubunge na udiwani

Imewekwa: September 13, 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imezipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 50 za wagombea ubunge na udiwani ambapo kati ya rufaa hizo 4 ni za wagombea ubunge na 46 ni za wagombea udiwani.

Haya yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Wilson Mahera Charles wakati akitangaza uamuzi wa kikao cha Tume kilichokutana jana tareje 12 Septemba.

Amesema kati ya rufaa hizo 50, Tume imekataa rufaa zote 4 za wagombea ubunge kutoka jimbo la Babati Mjini ambazo ni za wagombea ambao uteuzi wao ulitenguliwa, hivyo wagombea hao wanaendelea kutokuwa kwenye orodha ya wagombea.

“Aidha, Tume imezipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 46 za wagombea udiwani, imekubali rufaa 25 na kuwarejesha wagombea Udiwani katika orodha ya wagombea Udiwani.”, amesema Dkt. Charles.

Ametaka kata ambazo rufaa hizo zimetoka kuwa ni kata ya Changaa (Kondoa), Kichonda (Liwale), Kisima (Same Magharibi), Kibada (Kigamboni), Utende (Katavi), Myamba (Same Mashariki), Buswelu (Ilemela), Kiseke (Ilemela), Kimochi (Moshi Vijijini), Kikilo (Kondoa).

Kata nyingine ni Bereko (Kondoa), Isanga (Maswa Magharibi), Kirumba (Ilemela), Liwale Mjini (Liwale), Mshewe (Mbeya Vijijini), Nar (Babati Vijijini), Namiungo (Tunduru Kaskazini), Kimbiji (Kigamboni), Chitete (Ileje), Dunda (Bagamoyo), Kimambi (Liwale), Ludewa (Ludewa), Mwabusalu (Kisesa), Konje (Handeni Mjini) na kata ya Makurumla (Ubungo).

Dkt. Charlse ameongeza kuwa, Tume pia imekataa rufaa 12 za wagombea udiwani ambao hawakuteuliwa kutoka kwenye Kata za Mwayaya (Buhigwe), Bwakira Chini (Morogoro Kusini), Lalago (Maswa Mashariki), Duga (Tanga Mjini), Makurumla (Ubungo), na kata ya Ngoywa (Sikonge).

“Kata nyingine ni Isyesye (Mbeya Mjini), Iwambi (Mbeya Mjini), Oltrumet (Arumeru Magharibi), Iyunga (Mbeya Mjini), Bumilayanga (Mafinga Mjini) na Kahangara (Magu).”, amesema Dkt. Charles.

Katika hatua nyingine, Dkt. Charles amesema Tume pia imekataa rufaa 9 za kupinga wagombea Udiwani walioteuliwa kutoka kwenye Kata za Maendeleo (Mbeya Mjini), Forest (Mbeya Mjini), Kashaulili (Mpanda Mjini), Isanga (Mbeya Mjini), Mbalizi Road (Mbeya Mjini), Itende (Mbeya Mjini), Sinde (Mbeya Mjini), Boma (Mafinga Mjini) na Makuro (Singida Kaskazini).

Amefafanua kuwa idadi hiyo ya rufaa za wagombea ubunge zilizofanyiwa uamuzi na Tume zimefikia rufaa 117 na za wagombea udiwani zimefikia rufaa 195.

Dkt. Charles amesema kuwa Tume itaendelea kutoa matokeo baada ya usajili na uchambuzi wa rufaa hizo kila siku. Wahusika wa rufaa hizo watajulishwa kwa barua juu ya uamuzi wa Tume.

Habari Mpya

  • Tume yashiriki mkutano wa ECF SADC kuimarisha usimamizi wa uchaguzi na kujenga demokrasia nchini
    March 11, 2021
  • Tume yamtangaza Dkt. Magufuli kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Oktoba 28, 2020
    October 31, 2020
  • Tume yaongeza siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuapisha mawakala wa vyama vya siasa kwa ajili ya uchaguzi
    October 23, 2020

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Orodha ya Madiwani Wateule wa Viti Maalum walioteuliwa na Tume katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
  • Orodha ya Madiwani Wateule wa Viti Maalum wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2020
  • Orodha ya Wagombea wa Kiti cha Rais
  • Orodha ya Wagombea Ubunge
  • Wagombea waliopita bila kupingwa

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, Uchaguzi House, Njedengwa Investment Area, Block D, Plot No. 4
  • Namba ya Simu : +255 22 2114963-6
  • Nukushi : +255 22 2116740, +255 22 2127075
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2021 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi