• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume kuanza Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kuanzia Julai, 2019

Imewekwa: June 13, 2019

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) itaboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, awamu ya kwanza kuanzia mwezi Julai, 2019 kwa kutumia Teknolojia ya kieletroniki ya Biometriki (BVR).

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Mahakama ya Rufaa), Semistocles Kaijage wakati alipokutana na wakilishi wa Vyama vya Siasa vilivyopata Usajili wa Kudumu katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC) Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti, Jaji Semistocles Kaijage alisema kulingana na Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Kifungu cha 21 (5), sura 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali ya Mitaa Sura ya 292 Tume inapaswa kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara mbili katika Uchaguzi Mkuu mmoja na Uchaguzi Mkuu mwingine unaofuata.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili utafanyika baada ya kukamilika kwa uboreshaji awamu ya kwanza.

Mhe, Jaji Kaijage alisema kuwa uboreshaji huo unafanyika baada ya kukamilika kwa sehemu kubwa ya maandalizi ya uboreshaji wa Daftari kama uhakiki wa vituo vya kandikisha Wapiga Kura, uandikishaji wa majaribio wa Wapiga Kura katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, maandalizi ya vifaa vya Uboreshaji wa Daftari na mkakati wa Elimu ya Mpiga Kura.

Mwenyekiti alisema kuwa uandikishaji wa Wapiga Kura wa mwaka huu, 2019 Tume itaandikisha Wapiga Kura wapya na wale waliopoteza kadi za kupigia kura au kadi zao kuharibika, wanaorekebisha taarifa zao na bila kusahau waliohama kutoka maeneo yao ya awali na kuhamia maeneo mengine ya Uchaguzi tofauti na uandikishaji wa mwaka 2015 ambapo wapiga kura wote nchi nzima waliandikishwa.

Ili kuhamasisha wananchi wajitokeze kujiandikisha kwa wingi, Tume itatumia njia mbalimbali za Elimu ya Mpiga Kura kuwaelimisha kupitia Taasisi au Asasi za Kiraia zenye sifa ya kutoa elimu hiyo, kukutana na wananchi ana kwa ana kwa kushiriki maonyesho mbalimbali, mikusanyiko ya kijamii, gari la matangazo la Tume, Vyombo vya Habari, mitandao ya kijamii, Makala za magazeti na machapisho mbalimbali kama mabango na vipeperushi.

Mwenyuekiti pia aliwambia wawakilishi wa Vyama vya siasa kuleta majina ya mawakala wao Tume siku saba kabla ya Uboreshaji ili waapishwe kupata vibali kwa ajili ya kusimamia uandikishaji wa Wapiga Kura vituoni.

Mwaka huu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) itakuwa na vituo vya uandikishaji Wapiga Kura 37, 407 tofauti na vituo 36,549 vilivyotumika mwaka 2015 na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) itatumia vituo vya kuandikisha Wapiga Kura 407 tofauti na idadi ya vituo 380 vilivyotumika mwaka 2015.

Aidha, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Dkt. Athumani J. Kihamia alisema kuwa maeneo yanayokubalika kuwekwa vituoa vya uandikishaji Wapiga Kura kulingana na Kanuni ya 12 (2) ya Kanuni za Uboreshaji wa Daftari chini ya Sheria ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Kamuni ya 12 (2) ya Kanuni ya Uboreshaji wa Daftari chini ya Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 ni majengo ya umma na maeneo ya wazi yanayofikika kwa urahisi.

Pamoja na hayo, Mkurugenzi wa Uchaguzi alibainisha maeneo yasiyokubalika kwa mujibu wa Kanuni ya 12 (3) ya Kanuni za Uboreshaji wa Daftari ya Sheria ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Kanuni ya 15 (3) ya Kanuni za Uboreshaji wa Daftari chini ya Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 ni Kambi za Jeshi, Numba za Ibada na Ofisi za Vyama vya Siasa

Habari Mpya

  • Wadau wa Uchaguzi watakiwa kuwahamasisha wanachi kata ya ikoma wilayani Rorya kushiriki uboreshaji
    November 20, 2023
  • Tume yatangaza kuanza Uboreshaji wa Majaribio
    November 10, 2023
  • Tume yafanya Uteuzi wa Mbunge wa Viti Maalum
    November 03, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi