• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume ipimwe kutokana na utendaji kazi wake - Jaji Lubuva

Imewekwa: August 28, 2017

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwenye viwanja vya SabaSaba jijini Dar es Salaam amesema, licha ya kuwa Mwenyekiti na Wajumbe wengine wa Tume wanateuliwa na Rais, Tume imekuwa ikifanya kazi zake kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu yeyote, taasisi, au hata viongozi walioko madarakani.

Jaji Lubuva amesema kuwa uhuru wa Tume ambao Wananchi wengi wamekuwa wakiuzungumzia ni fikra tu za mtu anavyodhani juu ya namna Tume iundwe na si utendaji halisi wa Tume namna inavyotekeleza majukumu yake.

Ili kuondoa dhana hiyo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imependekeza katika katiba inayopendekezwa kuwa mfumo wa kuwapata Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ufanyiwe marekebisho ili kuwapata wajumbe kwa njia tofauti na ilivyo sasa.

Hata hivyo Jaji Lubuva ameshauri kuwa, Wajumbe wanaounda Tume ya Taifa ya Uchaguzi wasitokane na itikadi za vyama vya siasa ili kuepusha mgongano wa kimaslahi ambao unaweza kujitokeza katika utekelezaji wa majukumu hasa wakati wa kufanya maamuzi.

Akitolea mfano Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya, iliundwa kutokana na mapendekezo ya katiba mpya na kuitwa kuwa ni Tume huru lakini hivi sasa wale ambao hawakushinda katika Uchaguzi uliosimamiwa na Tume hiyo wameeleza kuwa Tume ya sasa ni mbaya zaidi kuliko iliyokuwepo hapo awali.

Mwenyekiti Lubuva ametoa wito kwa Wananchi wa Tanzania kuwa wasifikiri kuwa jina la Tume kuitwa huru ndio linaifanya Tume kuwa huru, bali uhuru wa Tume unatokana na utendaji kazi wake bila kuingiliwa na mtu, taasisi, au kiongozi yeyote aliyeko madarakani.

Jaji Lubuva ametembelea mabanda mbalimbali katika maonyesho ya SabaSaba yanayoendelea likiwemo banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jeshi la kujenga Taifa, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mahakama Kuu na Pride Tanzania.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi