• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

NEC YACHANGIA DAMU HOSPITALI YA UHURU DODOMA.

Imewekwa: June 21, 2022

Katika kuadhimisha wiki ya utumishi wa umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekuchangia damu na kufanya usafi katika Hospitali ya Uhuru iliyopo katika wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.

Watumishi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi wameshiriki utoaji wa damu ikiwa ni kuunga mkono jitihada za kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa, wakina mama wajawazito na watoto.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Chamwino Dkt. Abdul Pumzi amesema uhitaji wa damu katika hospitali zetu nchini ni mkubwa mno, hivyo amewapongeza watumishi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kujitoa kwao kwa kuchangia damu kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.

“Ni furaha kuwaona watumishi wa umma kama nyinyi mkishirki na kuunga mkono uchangiaji wa damu. Tumekuwa tukizunguka mijini na vijijini kuhimiza uchangiaji wa damu na hii ni kutokana na uhitaji wake kuwa mkubwa sana kwenye hospitali zetu. Kuna wa kina mama wajawazito, kuna majeruhi wa ajali mbalimbali, kuna watoto, wote hawa wana uhitaji wa damu, hivyo kuja kwenu hapa ni ishara ya moyo wa upendo” alisema Dkt.Pumzi.

Awali akizungumza na Watumishi wa Tume, Muuguzi Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Uhuru Bi. Joyce Nchimbi aliupongeza uongozi wa Tume kwa kuwafikiria na kufika katika hospitali hiyo na kushiriki zoezi la usafi na uchangiaji wa damu kama sehemu ya kuadhimisha kuadhimisha wiki ya utumishi wa Umma. Alitoa wito kwa taasisi na mashirika binafsi kujitoa kwa namna hiyo ili kuokoa maisha ya wagonjwa walio wengi katika hospitali zetu nchini.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa RasilimaliWatu kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Leonard Tumua amesema ushiriki wa watumishi katika uchangiaji wa damu na ufanyaji wa usafi katika wiki hii ya utumishi wa Umma unalenga kujenga mahusiano mema kati ya wadau ambao ni wananchi na Tume ya Taifa ya uchaguzi.

“Sisi kama Tume tunafanya kazi na wadau mbalimbali, hivyo kushiriki katika mazoezi kama haya, kunatuweka karibu na wadau wetu ambao ni wananchi, kunadumisha mahusiano mema na upendo miongoni mwetu sote” Alisema Bw.Tumua.

Nao baadhi ya watumishi kutoka Tume ya Taifa ya uchaguzi walioshiriki zoezi hilo wamesema, wamefurahishwa na uongozi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kuwaruhusu kushiriki zoezi la ufanyaji wa usafi lakini pia kutoa damu ikiwa ni ishara ya upendo wa watanzania waliopo hospitali na wenye uhitaji wa Damu.

“Tunashukuru sana uongozi wetu ukiongozwa na Dkt. Wilson Mahera Charles kwa kuona umuhimu wetu kama watumishi kushiriki katika shughuli za kijamii hasa uchangiaji wa Damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa.” alisema Bw. ErastoMwakalinga.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma imeanza Tarehe 16 mwezi Juni na inatarajia kumalizika Tarehe 23 mwezi Juni 2022 huku ikiwa na ujumbe “Nafasi ya Mapinduzi ya nne ya Viwanda katika masuala mapya yanayojitokeza kuhusu utoaji wa huduma na urejeshaji wakati na baada ya janga la Corona”.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi