• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Kamati ya Bunge yatembelea Ofisi za Tume ya Tiafa ya Uchaguzi zilizoo Njedengwa jijini Dodoma

Imewekwa: October 25, 2021

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Nagy Kaboyoka, imetembelea Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuona Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika eneo la Njedengwa Jijini Dodoma.

Kamati hiyo ya Bunge kwa pamoja imefurahishwa sana na mradi wa Ujenzi wa Ofisi hizo za Tume zilizoko katika eneo la Njedengwa JijiniDodoma. Ambao kwa asilimia kubwa umekamilika.

Mkurugenzi wa Uchaguzi, Dkt. Wilson Mahera Charles akiielezea Kamati hiyo kabla ya kuitembeza kwenye Ofisi za Tume na maandhali ya kuvutia ya nje, alisema kuwa ofisi za Tume zina Majengo matatu ambayo ni Jengo la Utawala (Main Building), Jengo la Kuhifadhia Vifaa (Warehouse) na Jengo la kutangazia matokeo (Results Center)

Mkurugenzi alifafanuwa kuwa kwa ujumla ujenzi wa majengo yote matatu unaendelea vizuri kwani majengo yako katika hatua mbalimbali ambapo hadi sasa Jengo la Utawala limekamilika kwa asilimia 99 na makabidhiano ya awali yalifanyika tarehe 22 Julai, 2020, Jengo la Kuhifadhia Vifaa asilimia 99 na Jengo la kutangazia matokeo kwa asilimia 97.

Aidha, Mkurugenzi aliielezea Kamati hiyo ya Bunge kuwa Jengo la Utawala na Jengo la Kuhifadhia Vifaa yameshaanza kutumika na inaendelea na ukamilishaji wa shughuli nyingine zinazotekelezwa na wazabuni mbalimbali.

“Tume inaishukuru serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hizi na hivyo kufanikisha Tume kuwa na majengo yake Dodoma na kwa ujumla, ujenzi wa majengo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi unaelekea kukamilika kwani umeshafikia hatua ya kumalizia shughuli ndogondogo ambazo zinatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 30, 2021 na hadi sasa mradi huu umegharimu jumla ya kiasi cha Shilingi 19,713,413,335.44 “ Alisema Mkurugenzi wa Uchaguzi

Pamoja na hayo, Mkurugenzi wa Uchaguzi aliielezea Kamati ya Bunge kuwa Tume ina uhitaji wa Ujenzi wa ofisi ndogo Jijini Dar es Salaam katika eneo lake lililopo Garden Avenue.

Mkurugenzi alifafanua kuwa ni muhimu kuwa na ofisi ndogo Dar-es-Salaam kwakuwa Tume inafanya kazi na wadau wengi ambao bado wapo Dar-es-Salaam na vifaa vingi vya uchaguzi huwa vinashushwa katika bandari ya Dar-es-Salaam.

Zaidi ya hayo, Charles alisema kuwa Tume inauhitaji wa kutatafuta eneo lililokaribu na reli ya SGR ili kujenga maghala mengine Dodoma kwa ajili ya kuiwezesha Tume kuhifadhi vifaa vyake vyote.

Habari Mpya

  • Tume yashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar
    January 02, 2023
  • Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa kushiriki Uchaguzi Mdogo Jimbo la Amani na Kata Saba
    December 16, 2022
  • Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa kushiriki Uchaguzi Mdogo Jimbo la Amani na Kata Sita za Tanzania Bara
    December 16, 2022

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Mpango Mkakati wa NEC 2021/22 – 2025/26
  • Taarifa ya Tathmini ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2020
  • Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa mwaka 2020
  • Wabunge Wanawake Walioteuliwa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi