• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Tume yamtangaza Dkt. Magufuli kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Oktoba 28, 2020

Imewekwa: October 31, 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imemtangaza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata kura nyingi halali kuliko wagombea wengine na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM katika Uchaguzi wa Rais uliofanyika tarehe 28 Oktoba mwaka huu.

Hayo yametangazwa jijini Dar es Salaam tarehe 30 Oktoba, 2020 na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Rufaa Mst. Semistocles Kaijage baada ya kukamilika kwa utangazaji wa matokeo ya kura za Rais katika majimbo yote 264.

Jaji Kaijage amesema mgombea huyo wa CCM amepata kura 12,516,252 kati ya kura halali 14,830,195 zilizopigwa na idadi halisi ya waliopiga kura 15,091,950 kati ya wapiga kura 29,754,699 walioandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapig Kura la Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na walioandikishwa kwenye Daftaria la Kudumu la Wapiga Kura la Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC).

Amewataja wagombea wengine kutoka vyama 14 vilivyoshiriki katika uchaguzi wa Rais na kura walizopata kwenye mabano kuwa ni Mahona Leopold Lucas wa NRA (80,787), Shibuda John Paul wa chama ADA TADEA (33,086) na Muttamwega Bhatt Mgaywa wa chama cha SAU (14,922).

Amewataja wagombea wengine ni Cecilia Augustino Mmanga wa Chama cha Demokrasia Makini aliyepata kura 14, 556, Maganja Yeremia Kulwa wa Chama cha NCCR Mageuzi amepata kura 19,969, Lipumba Ibrahim Haruna wa Chama cha CUF amepata kura 72,885.

Jaji Kaijage ameongeza kuwa mgombea Philipo John Fumbo kutoka Chama cha DP amepata kura 8,283, Membe Bernard Kamillius wa Chama cha ACT-Wazalendo amepata kura 81,129, Queen Cuthbert Sendiga wa Chama cha ADC amepata kura 7,627.

“Mgombea Twalid Ibrahim Kadege wa Chama cha UPDP amepata kura 6,194, Rungwe Hashim Spunda wa Chama cha CHAUMA amepata kura 32,878, Mazrui Khalfani Mohamed wa Chama cha UMD amepata kura 3,721, Seif Maalim Seif wa Chama cha AAFP amepata kura 4,635 na Lissu Tundu Antiphas Mughwai wa Chama cha CHADEMA amepata kura 1,933,271”, amesema Jaji Kaijage.

Baada ya kutangaza matokeo hayo mawakala 12 wa vyama vya siasa kati ya mawakala wa vyama vilivyoshiriki katika uchaguzi wa Rais walisaini Fomu Namba 27, kati ya mawakala 13 waliokuwepo wakati wa kutangazwa matokeo hayo.

Jaji Kaijage amesema ametangaza matokeo hayo kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 38 (1), Ibara ya 41 (6) na Ibara ya 47 (2) za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa pamoja na Kifungu cha 35 (f) (8) na Kifungu cha 35 (h) vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 ya Sheria za Tanzania.

Mbali na kura halali zilizohesabiswa, Jaji Kaijage amesema idadi ya kura zilizokataliwa ni kura 261,755.

Amesema baada ya kutangaza matokeo hayo ya uchaguzi wa Rais, siku ya Jumapili Tume ya Taifa ya Uchaguzi itatoa hati ya ushindi kwa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais walioshinda.

Habari Mpya

  • Tume yashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar
    January 02, 2023
  • Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa kushiriki Uchaguzi Mdogo Jimbo la Amani na Kata Saba
    December 16, 2022
  • Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa kushiriki Uchaguzi Mdogo Jimbo la Amani na Kata Sita za Tanzania Bara
    December 16, 2022

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Mpango Mkakati wa NEC 2021/22 – 2025/26
  • Taarifa ya Tathmini ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2020
  • Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa mwaka 2020
  • Wabunge Wanawake Walioteuliwa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi