Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewataka wadau wa uchaguzi kufikisha ujumbe sahihi kwa wananchi wa Kata ya Ikoma ili wajitokeze kwa wingi kushiriki uboreshaji wa majaribio wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuwabainisha waliopoteza sifa za kuwa wapiga kura.
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inatarajia kufanya zoezi la uboreshaji wa majaribio wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Kata ya Ng’ambo iliyopo katika Manispaa ya Tabora, Mkoani Tabora na Ikoma iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Mkoani Mara.
?Tume ya Taifa ya Uchaguzi imemteua Ndugu Aziza Sleyum Ally kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)
?Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbarali, Bw. Missana Kwangura amemtangaza Bi. Bahati Ndingo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa mshindi wa kiti cha Ubunge wa Jimbo hilo baada ya kupata kura 44,334 kati ya kura 56,095 halali zilizopigwa kwenye vituo 490 vya kupigia kura.
?Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo tarehe 19 Septemba, 2023 ametembelea na kukagua zoezi la kupiga kura kwenye Jimbo la Mbarali lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.