Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
TIMU ya Kamba ya Tume ya Aifa ya Uchaguzi (NEC) imefanikiwa kutwaa kombe katika Bonanza la Ukaguzi lililofanyika Jijini Dodoma na kushirikisha timu zaidi ya sita.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mara ya kwanza inashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayofanyika kwenye viwanja vya Maisara Unguja kwa kutoa Elimu ya Mpiga Kura kwa wananchi wanaotembelea banda la Tume.
Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wanatarajiwa kushiriki katika uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Amani Mkoa wa Mjini, Zanzibar na Kata saba za Tanzania Bara tarehe 17 Desemba, 2022.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imepitia, kuchambua na kufanya uamuzi wa rufaa tatu na kuwarejesha wagombea Udiwani katika Uchaguzi Mdogo wa Ubunge na Udiwani unaotarajia kufanyika tarehe 17 Desemba mwaka 2022.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetoa vibali vya kutoa Elimu ya Mpiga Kura kwa Taasisi au Asasi tatu za Kiraia kwenye Uchaguzi Mdogo wa Udiwani katika Kata tatu za Tanzania Bara.