• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume yatwaa Kombe Mchezo wa Kuvuta Kamba kwenye Bonanza la Ukaguzi

Imewekwa: March 20, 2023

TIMU ya Kamba ya Tume ya Aifa ya Uchaguzi (NEC) imefanikiwa kutwaa kombe katika Bonanza la Ukaguzi lililofanyika Jijini Dodoma na kushirikisha timu zaidi ya sita.

NEC ilitwaa ushindi huo baada ya kuwavuta kwa mivuto miwili Timu ya Ukaguzi.


Katika Mpira wa Miguu NEC hawakufurukuta mbele ya Makao Makuu Jogging baada ya kuwatupa nje kwa mikwaju ya penati ambao badae katika fainali walikutana Ugakuzi na Makao Makuu na Makao Makuu kutwaa ubingwa wa Soka.


Katika mchezo wa Mpira wa Netball timu ya Ukaguzi iliibuka kidedea baada ya kuwatndika bila huruma timu za Wizara ya Afya na Madini.


Mapema akizungumza wakati wa ufunguzi wa bonanza hilo, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere ametoa rai kwa watumishi wa umma wakiwemo wa Ofisi yake kushiri kwenye michezo kwani ni tiba isiyo na gharama.


Taasisi zilizoshiriki mbali na watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mfuko wa Bima ya Afya ya Uchaguzi(NHIF), Wakala wa Barabara(Tanroads) Ofisi ya Rais Ikulu na Wizara ya Afya.


Alisema ili kuwa na afya njema ni vyema watumishi wakashiriki mazoezi na kusisitiza kuwa mazoezi ni tiba isiyo na gharama kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza na pia kuipunguzia Serikali mzigo wa kuhudumia magonjwa hayo.


"Kazi zetu sisi Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali tunatumia muda mwingi kuandika taarifa hivyo tumekuwa tukiweka utaratibu wa kutoka nje kufanya mazoezi na ni utaratibu mzuri katika kulinda afya za watumishi."


Kichere pia alisema wanatumia bonanza hilo kujiandaa tayari na bonazan lingine litakalokutanisha na wabunge.


" Wabunge ni watu ambao tunafanya kazi nao kwa karibu, hivyo mwezi ujao tutakuwa na bonanza la kushirikiana na wabunge kwa hiyo hii ni sehemu ya mazoezi yetu."


Kichere alisema katika bonanza Hilo pia watalitumia kuchagia damu benki ya Taifa ya damu Ili kusaidia kutoka maisha ya watu wanaohitaji damu.


Naye Mkurugenzi wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya CAG, Novat Mfalamagoha kutokana na mtindo wa maisha ya mwanadamu mazoezi ni mabadala mzuri wa dawa za hospitali.


Pia alishauri wazazi kujenga tabia ya kuwashirikisha watoto kwenye mazoezi ambayo itawafanya kujenga moyo wa kupenda mazoezi.

Habari Mpya

  • Wadau wa Uchaguzi watakiwa kuwahamasisha wanachi kata ya ikoma wilayani Rorya kushiriki uboreshaji
    November 20, 2023
  • Tume yatangaza kuanza Uboreshaji wa Majaribio
    November 10, 2023
  • Tume yafanya Uteuzi wa Mbunge wa Viti Maalum
    November 03, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi