• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano

Tume yashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Imewekwa: January 02, 2023

Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mara ya kwanza inashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayofanyika kwenye viwanja vya Maisara Unguja kwa kutoa Elimu ya Mpiga Kura kwa wananchi wanaotembelea banda la Tume.

Maonesho hayo yameanza tarehe 1 Januari mwaka 2023 hadi siku ya kilele cha Sherehe za Mapinduzi tarehe 12 Januari mwaka 2023 huku taasisi mbalimbali za Serikali zikishiriki maonesho hayo ambapo Kaulimbiu ya sherehe inasema Mapinduzi Yetu Ndio Amani Yetu, Tuyalinde kwa Maendeleo Yetu.

Katika maonesho hayo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inatoa Elimu ya Mpiga kura kwa kukutana na wananchi ana kwa ana na kuwapa elimu, kujibu maswali mbalimbali ya wadau wa Uchaguzi kuhusu masuala ya kiuchaguzi na kugawa vipeperushi kwa wananchi wanaotembelea banda la Tume.

Hata hivyo, Sherehe za mwaka huu za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar zinazonogeshwa na mashindano ya Kombe la Mapinduzi, hazitafanyika baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi kufuta sherehe hizo.

Akizungumzia suala hilo Dkt. Mwinyi alisema fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe hizo za miaka 59 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar Shilingi Milioni 450 zitatumika kujenga madarasa, kuongeza madawati, maabara na huduma nyingine za sekta ya elimu visiwani Zanzibar.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inashiriki kwenye maonesho hayo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa matakwa ya Kifungu cha 4C cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 kinachoipa mamlaka Tume kutoa Elimu ya Mpiga Kura nchi nzima na kuratibu watu wanaotaka kutoa elimu hiyo.

Habari Mpya

  • Tume yatwaa Kombe Mchezo wa Kuvuta Kamba kwenye Bonanza la Ukaguzi
    March 20, 2023
  • Tume yashiriki Maonesho ya Sherehe za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar
    January 02, 2023
  • Wapiga Kura 114,647 walioandikishwa kushiriki Uchaguzi Mdogo Jimbo la Amani na Kata Saba
    December 16, 2022

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Mpango Mkakati wa NEC 2021/22 – 2025/26
  • Taarifa ya Tathmini ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2020
  • Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa mwaka 2020
  • Wabunge Wanawake Walioteuliwa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi