• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume yafanya uamuzi wa rufaa 616 zilizowasilishwa na wagombea ubunge na udiwani

Imewekwa: September 18, 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imefanya uamuzi wa rufaa 616 za wagombea ubunge na udiwani katika Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Oktoba 28, 2020.

Hayo yamsemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa tume hiyo Dkt. Wilson Mahera Charlse wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu uchambuzi na uamua wa rufaa za wagombea wa ubunge na Udiwani.

Amesema hadi kufikia jana tarehe 17 Septemba, 2020, baada ya kupitia kumbukumbu zote za rufaa zilizowasilishwa, Tume imepokea jumla ya rufaa 616 zikiwemo za ubunge rufaa 160, udiwani rufaa 456, malalamiko 25 na rufaa zilizojirudia 44.

“Katika rufaa 160 za ubunge zilizoamuliwa na Tume matokeo yake ni wagombea waliorejeshwa ni 66, wagombea ambao hawakurejeshwa ni 32, rufaa zilizokataliwa za kuomba kuenguliwa wagombea 57 na rufaa zilizojirudia ni 5.

Dkt. Charles ameongeza kuwa baada ya Tume kupitia rufaa zilizowasilishwa kutoka katika majimbo hayo, imerejesha wagombea 3 waliokuwa wameenguliwa katika majimbo ya Namtumbo, Bukene na Kavuu.

Amesema kutokana na uamuzi huo majimbo hayo matatu yataendelea na kampeni na uchaguzi utafanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

“Baada ya kupitia na kuamua rufaa mbalimbali, Tume imekubali rufaa tatu (3) na kuwaengua wagombea katika majimbo matatu. Kwa matokeo hayo wabunge waliopita bila kupingwa ni 18”, amesema Dkt. Charles na kuongeza kuwa:

“Pia, Tume imepokea taarifa ya kujitoa kwa wagombea wa Ubunge kwenye Majimbo ya Chalinze na Madaba, hivyo kubakia wagombea pekee ambao wanakuwa wamepita bila kupingwa”.

Amesema kufuatia kumalizika kwa kipindi cha pingamizi na rufaa, wagombea waliopita bila kupingwa kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 ni 20.

Amefafanua kuwa Tume itawatangaza katika Gazeti la Serikali kwa mujibu wa sheria.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi