• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi Mkuu
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Maadili ya Uchaguzi
    • Rufaa za Uchaguzi Mdogo 2021
    • Miongozo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
    • Orodha ya Matokeo ya Rufaa za Ubunge zilizoamuliwa na Tume
    • Wagombea waliopita bila kupingwa
    • Wagombea katika Uchaguzi Mkuu 2020
    • Wabunge na Madiwani Wateule wa Viti Maalum Uchaguzi Mkuu 2020
    • Jarida la Tume kuhusu Uchaguzi Mkuu 2020
    • Mpango Mkakati wa NEC 2021/2022 – 2025/2026
    • Kura ya Maoni
    • Maelekezo
    • Orodha ya Majimbo na Kata
  • Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • NEC Online TV
    • Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Ratiba ya Kampeni za Wagombea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020
    • Voters Interaction System
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida la Tume la Uchaguzi Mkuu 2020
  • Zabuni/Mnada
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Jarida la Uchaguzi

Tume yaongeza siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuapisha mawakala wa vyama vya siasa kwa ajili ya uchaguzi

Imewekwa: October 23, 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeongeza siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi katika majimbo yote nchini kuapisha mawakala wa vyama vya saisa kwa ajili ya siku ya uchaguzi tarehe 28 Oktoba, 2020.

Uamuzi huo umetangazwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa tume hiyo Dkt. Wilson Mahera Charles wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Dkt. Charles amesema siku hizo tatu ni kuanzia tarehe 21 hadi 23 Oktoba, 2020 na uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao cha Tume kilichokaa siku ya jumatano tarehe 21 Oktoba, 2020.

Amesema Tume imefanya uamuzi huo kwa kuzingatia mamlaka iliyopewa na Kifungu cha 57 (2) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 ikisomwa pamoja na Kifungu cha 58 cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292.

Ameongeza kuwa uamuzi huo umefikiwa kutokana na baadhi ya maeneo kuwa na changamoto ya kutofikika kwa urahisi kutokana na jiografia na hivyo kuwa vigumu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuwafikia na kuwaapisha mawakala hao kwa mujibu wa sheria.

Hata hivyo, Dkt. Charles alivitaka vyama vya saisa vipeleke orodha ya mawakala wao na viwe vimewapanga mawakala hao katika vituo vya kupigia kura na kuweka anuani au namba ya simu ya kila wakala husika.

“Lakini tunaviasa vyama vya saisa kupeleka mawakala kwa utaratibu unaokubalika na iwapo vitapeleka mawakala wasiohusika au kuwapeleka kwenye eneo ambalo sio lao na bila kufuata utaratibu wanaweza kujikuta wako matatani”, amesema Dkt. Charles na kuongeza:

“Ila ni matarajio ya Tume kuwa hii kazi ya kuwaapisha mawakala wa vyama vya siasa litaendelea kufanyika kwa utaratibu mzuri ambapo wasimamizi wa uchaguzi watatenga maeneo katika jimbo ambayo yanafikika kiurahisi”

Dkt. Charles amevitaka vyam vya siasa kufuata utaratibu wa kisheria na kwa mujibu wa maelekezo kwa vyama vya siasa na wagombea vitapata fursa kwa mawakala wao kuapishwa.

Amefafanua kuwa mawakala wa vyama 19 vya siasa vyenye usajili wa kudumu wanatarajiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na Urais.

Habari Mpya

  • Tume yatangaza matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Mbarali na Kata Sita za Tanzania Bara
    September 21, 2023
  • ?Mwenyekiti wa Tume Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele atembelea na kukagua Uchaguzi Mdogo Jimbo la Mbarali
    September 19, 2023
  • Wapiga kura 216,282 kupiga kura uchaguzi mdogo wa Mbarali na kata sita
    September 19, 2023

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Jarida la Uchaguzi, Agosti, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Julai, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Machi, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Februari, 2023
  • Jarida la Uchaguzi Toleo la Januari, 2023
Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 358, Dodoma, The National Electoral Commission, 5 Uchaguzi Road, 41107 Njedengwa Uchaguzi House
  • Namba ya Simu : +255 26 2962345-8
  • Nukushi : +255 26 2962348
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume.
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2023 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi