• English
  • |
  • Maswali yaulizwayo Mara kwa Mara   |  
  • Staff Mail

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Uchaguzi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Wajumbe wa Tume
    • Dira na Dhima
    • Jinsi NEC Ilivyoanzishwa
  • Uchaguzi
    • Mifumo ya Uchaguzi
    • Mzunguko wa Uchaguzi
    • Uchaguzi Mkuu
    • Uchaguzi Mdogo
    • Matokeo ya Uchaguzi
    • Kura ya Maoni
  • Wapiga Kura
    • Vituo vya Uandikishaji
    • Takwimu za Wapiga Kura
    • Elimu ya Mpiga Kura
    • Uhakiki
  • Machapisho
    • Sheria za Uchaguzi
    • Kanuni za Uchaguzi
    • Ripoti
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Taarifa wa Umma
    • NEC Online TV
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
  • Zabuni
    • Zabuni za Ndani
    • Zabuni za Kimataifa
  • Mawasiliano
  • Blogu ya Tume

Wasimamizi wa Uchaguzi Mdogo watakiwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu

Imewekwa: October 03, 2018

Wasimamizi wa Uchaguzi mdogo wa Ubunge na Udiwani utakaofanyika Oktoba 13 mwaka huu katika jimbo la Liwale na kwenye Kata 37 za Tanzania Bara wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia matakwa ya Katiba, Sheria na Kanuni za uchaguzi.

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mbarouk Salim Mbarouk ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku 3 kwa Wasimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi kutoka katika maeneo yenye uchaguzi.

Jaji Mbarouk amewataka Wasimamizi hao kufanya kazi kwa ufanisi, uhuru, uwazi na bila kuegemea upande wowote ili uchaguzi huo ufanyike kwa amani na utulivu.

Amesema uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbalimbali zinazopaswa kufuatwa na kuzingatiwa akisisitiza kwamba hatua na taratibu hizo ndiyo msingi wa uchaguzi mzuri wenye ufanisi usio na malalamiko au vurugu.

“ Tunakutana hapa ili kwa pamoja tubadilishane uzoefu, tujadili namna ya kufanikisha zoezi la uchaguzi lakini pia namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokeza katika hatua zote za uchaguzi, natumaini mtatumia fursa hii kubadilishana uzoefu katika kutekeleza jukumu hili lililo mbele yenu” Amesema Jaji Mbarouk.

Jaji Mbarouk ametoa wito Wasimamizi hao waepuke madhara yanayotokana na ukiukaji wa Sheria, Kanuni na taratibu za Uchaguzi akisisitiza kwamba katika kipindi hiki chaguzi zinafanyika katika mazingira ambayo yana hamasa kubwa ya Kisiasa, kutoaminiana na wakati mwingine kutawaliwa na mihemko ambayo imekuwa chanzo cha uvunjifu wa amani.

Aidha, amewaeleza Wasimamizi hao kuwa wameaminiwa na kuteuliwa katika nafasi hizo kwa kuwa wanao uwezo mkubwa wa kufanya kazi hivyo wajiamini na kujitambua.

Ametoa wito kwa Wasimamizi hao kuhakikisha kwamba wanayaelewa vema maeneo yao ya kazi na wanawatumia vyema wasaidizi walio nao katika maeneo yao ya kazi kwa matokeo bora.

“Naomba mjue mna jukumu la kuimarisha imani ya wananchi pamoja na wadau wote wa uchaguzi kwa Tume. Hivyo mfanye kazi kwa ufanisi wa hali ya juu, bila kuegemea upande wowote.Kufanya kazi kwa uhuru na kwa uwazi kutasaidia kudumisha amani katika maeneo yenu ya Uchaguzi” Amesema.

Kuhusu kufanyika kwa Uchaguzi huo mdogo Oktoba 13 mwaka huu, Jaji Mbarouk amesema kuwa kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 37 (1) (b) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343 kikisomwa pamoja na kifungu cha 13(3) cha Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura 292, ni jukumu la Tume kusimamia, kuendesha na kuratibu uchaguzi wa kujaza nafasi zilizo wazi.

Amesema kwa nyakati tofauti Tume imepokea taarifa kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye kwa kuzingatia Kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343 aliitaarifu Tume uwepo wa nafasi wazi za Ubunge katika jimbo la Liwale.

Pia amefafanua kuwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa, ambaye kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali ya Mitaa, Sura, 292 alitoa taarifa ya uwepo wa nafasi wazi za Madiwani katika Kata 37 kutoka katika Halmashauri 27 zilizopo katika Mikoa 13 ya Tanzania Bara.

Katika hatua nyingine Makamu Mwenyekiti huyo wa NEC Jaji Mbarouk Salim Mbarouk ameeleza kuwa jumla ya wagombea 6 waliteuliwa kugombea ubunge katika jimbo la liwale ambapo mgombea mmoja alijitoa baada ya uteuzi huo kukamilika.

Ameongeza kuwa katika Kata 37 za Tanzania Bara jumla ya wagombea 56 waliteuliwa kugombea udiwani katika Kata hizo.

Habari Mpya

  • Jaji Kaijage : Wananchi jitokezeni kupiga kura uchaguzi mdogo wa udiwani kata 3 za Tanzania Bara.
    January 28, 2019
  • Tume yatangaza Uchaguzi mdogo katika Kata ya Biturana na Mwanahina
    December 18, 2018
  • Tume yawataka Wasimamizi wa Uchaguzi kuzingatia Sheria na Taratibu za Uchaguzi
    December 11, 2018

Nifanyaje?

  • Kujiandikisha Kupiga Kura
  • Kupiga Kura

Machapisho

  • Uchaguzi Mkuu wa 2015
  • Safu ya Menejimenti
  • Uchaguzi wa Madiwani Mwaka 1994
  • Uchagzi Mkuu wa Mwaka 1985
  • Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge wa Mwaka 1980

Mawasiliano yetu

  • Address : P.O.Box 10923, Dar es Salaam, Ghana and Ohio Street
  • Namba ya Simu : +255 22 2114963-6
  • Nukushi : +255 22 2116740, +255 22 2127075
  • Barua Pepe : uchaguzi@nec.go.tz
  • Tovuti : www.nec.go.tz

Linki za Haraka

  • Maktaba ya Tume
  • Majukumu ya Msingi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Msajili wa Vyama vya Siasa

Kuwa karibu nasi

Jiunge na orodha ya baruapepe zetu ili uhabarishwe na kupata notisi kuhusu taarifa zetu mpya

Tufuatilie

@2019 Tume ya Taifa ya Uchaguzi . Haki zote zimehifadhiwa

  • Ramani ya Tovuti
  • Wasiliana Nasi