Habari

Uteuzi wa Wagombea Urais

Imewekwa: 2015-08-21 18:08:46

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeteua wagombea wa Urais kutoka vyama nane ambao wametimiza vigezo vilivyowekwa na Tume walioomba nafasi ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Jumla ya Vyama Kumi na vitatu (13) vilichukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea Urais katika Ofisi za Tume ya Makao Makuu ya Tume tangu zoezi hilo lilipoanza rasmi Agosti 1,2015.

Wagombea wa Urais waliochukua fomu walitakiwa kutimiza matakwa ya kisheria ikiwa ni pamoja na kupata wadhamini wasiopungua mia mbili (200) waliojiandikisha Kupiga Kura kila mkoa kwa mikoa kumi kati ya hiyo,miwili iwe ya Tanzania Zanzibar, pamoja na kuweka dhamana ya shilingi milioni moja na kula kiapo mbele ya Jaji wa Mahakama.

Hadi kufikia Saa kumi kamili jioni ya leo tarehe 21 mwezi Agosti, 2015 jumla ya Vyama tisa (9) Vilikuwa vimewasilisha fomu zikiwa zimekidhi vigezo vilivyotajwa na kwa hatua hiyo Wagombea wao kuteuliwa rasmi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa wagombea halali wa Nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vyama vilivyokuwa vimewasilisha fomu katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi hadi kufikia saa kumi kamili jioni ni kama ifuatavyo:

1. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

2. Chama cha Mapinduzi (CCM)

3. Chama cha Tanzania Labour Party (TLP)

4. Chama cha Alliance Democratic (ADC)

5. Chama cha United People’s Democratic Party (UPDP)

6. Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA)

7. Chama cha Alliance for Change and Transparent (ACT-WAZALENDO)

8. National Reconstruction Alliance (NRA)

9. Chama cha African Democratic Alliance (ADA-TADEA)

Kwa hatua hii na kwa mujibu wa Sheria, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inawatangaza Wagombe wafuatao pamoja na Vyama vyao kuwa ndio Wagombea Halali wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania:

1. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

Mhe. Edward Ngoyai Lowassa

2. Chama cha Mapinduzi (CCM)

Mhe. John Pombe Magufuli

Samia Suluhu Hassan

3. Chama cha Tanzania Labour Party (TLP)

Machmillan Elifatio Lyimo

4. Chama cha Alliance Democratic (ADC)

Chief Lutalosa Yembe

Mhe. Said Miraj Abdallah

5. Chama cha United People Democratic Party (UPDP

Mhe. Fahmi Nassoro Dovutwa

Hamadi Mohammed Ibrahimu

6. Chama cha UMMA (CHAUMMA)

Hashim Rungwe Spunda

Issa Abas Hussein

7. Chama cha Alliance for Change and Transparent (ACT-WAZALENDO)

Anna Elisha Mghwira

Hamad Mussa Yussuf

8. National Reconstruction Alliance (NRA)

Janken Malik Kasambala

Simai Abdulrahman Abdulla

Kwa kuzingatia Idadi ya Vyama vilivyochukua fomu ambavyo ni kumi na vitatu, dhidi ya vyama tisa (9) vilivyorejesha fomu ndani ya muda yaani kati ya saa 1.30 asubuhi na saa 10.00 jioni, vyama viwili vimeshindwa kurejesha fomu kwa wakati wakati ambapo vyama vingine viwili vimeshindwa kukamilisha masharti.

Chama cha Kijamii (CCK) na Chama cha African Democratic Alliance Party (ADA-TADEA) vimerejesha fomu lakini havikuweza kukidhi matakwa kwa mujibu wa sheria wakati Chama cha Haki na Ustawi (CHAUSTA) na Chama cha Democratic Party (DP) havikurejesha kabisa fomu.

Kwa Chama cha CCK kimeshindwa kukamilisha fomu namba 8 inayoonyesha idadi ya wadhamini wanaotakiwa kwa mujibu wa sheria. Aidha Chama cha ADA TADEA hakikukamisha sharti la Mgombea Mwenza kula kiapo.

Chama cha DP kimeshindwa kukidhi vigezo ikiwemo kuwa na Mgombea Mwenza pamoja na kulipa dhamana inayotakiwa.