The National Electrol Commission of Tanzania - Homepage
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YAKUTANA NA VIONGOZI WA MADHEHEBU YA DINI KUZUNGUMZIA UCHAGUZI MKUU

Home » Speeches
Speeches
  email E-mail this to a friend email Printable version

MKURUGEZI WA UCHAGUZI ATOA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UGAWAJI WA MAJIMBO YA UCHAGUZI WA WABUNGE

                                         JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
                                      TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UFAFANUZI KUHUSU UGAWAJI WA MAJIMBO YA UCHAGUZI WA WABUNGE
 
Kwa mujibu wa Ibara ya 75(1)(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ndiyo yenye mamlaka ya kuchunguza mipaka na kugawa majimbo ya Uchaguzi kwa ajili ya Uchaguzi wa Wabunge na siyo chombo kingine chochote.
 
Itakumbukwa kuwa tarehe 22/01/2010, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilitoa taarifa katika Vyombo vya Habari ikielezea nia yake ya kuchunguza mipaka na kugawa Majimbo kwa ajili ya Uchaguzi wa Wabunge. Katika maelezo yake, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilibainisha Vigezo na Utaratibu utakaotumika katika kuleta maombi kwa ajili ya kurekebisha mipaka au kugawa Majimbo. Taarifa hiyo pia  ilieleza hatua zitakazofuata baada Tume kupokea maombi.
 
Katika utaratibu ulioainishwa wa kuleta maombi ya kurekebishiwa mipaka au kugawanya majimbo, Tume ilizielekeza Halmashauri kufanya vikao rasmi na kushirikisha wadau wote katika eneo la Halmashauri husika ili kupata maoni na mapendekeza kutoka kwa wadau na kisha Mkurugenzi wa Halmashauri husika kuwasilisha maoni na mapendekezo ya wadau hao katika Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa. Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa kinatakiwa kuchambua maoni na mapendekezo hayo na kisha kuyawasilisha Tume.  Taarifa ilieleza mwisho wa kupokea mapendekezo hayo ni tarehe 28/02/2010.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kupitia magazeti mbalimbali imeona baadhi ya Halmashauri zimechapisha mapendekezo ya ugawaji wa Majimbo mapya kwenye magazeti, kitu ambacho kinawapa picha Wananchi kuwa Majimbo hayo yameshagawiwa tayari.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwaarifu Wananchi wote kwamba majimbo hayo bado hayajagawiwa kwa kuwa Chombo pekee kinachohusika na ugawaji wa Majimbo ni Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Aidha, Tume inapenda kuwaarifu wananchi wote kuwa bado inaendelea kupokea maombi ya mapendekezo ya kurekebisha mipaka au kugawa majimbo kutoka kwenye Halmashauri mbalimbali. Tume ikishapokea maombi hayo itayafanyia uchambuzi kulingana na vigezo na utaratibu uliowekwa. Majimbo yatakayokidhi vigezo yatashindanishwa tena kwa kuzingatia nafasi za viti zitakazoweza kuongezwa katika ukumbi wa Bunge.
 
Tume inawaomba Wananchi wafahamu kuwa mpaka sasa hakuna ugawaji wa Majimbo wowote ambao umeshafanyika. Tume itafanya ugawaji wa majimbo baada ya kupokea na kuyachambua maombi kutoka kwa Makatibu Tawala wa Mikoa. Tume ikikamilisha zoezi hilo itawatangazia wananchi na kuwaarifu kuhusu majimbo mapya yatakayoanzishwa.
 
Tume inawaomba Wananchi wote kuvuta subira ili mchakato wa zoezi hili uweze kutekelezwa kwa mujibu wa Sheria za Nchi na taratibu zilizowekwa.
 
                       (Rajabu R. Kiravu )
                   MKURUGENZI WA UCHAGUZI

  email E-mail this to a friend email Printable version

 

 

image Election Results Database
 
Election Type
Election Year
Region
District
Consituency
Ward
 
   
image Elected Candidate Profile
ABDULRASUL AZIZ ROSTAM [CCM]
IGUNGA Constituency
More Elected Candidate>>

image Registration Status

image

Click appropriate link to view your status

Email
image Election Results in Map Presentation


Click to view Election Results
image Visitors at this site
There have been 431625 visitors to this websiteThere have been 431625 visitors to this websiteThere have been 431625 visitors to this websiteThere have been 431625 visitors to this websiteThere have been 431625 visitors to this websiteThere have been 431625 visitors to this website
User online : 14
images Speeches
MKURUGEZI WA UCHAGUZI ATOA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UGAWAJI WA MAJIMBO YA UCHAGUZI WA WABUNGE
HOTUBA YA MAKAMU MWENYEKITI KATIKA UFUNGUZI WA MKUTANO WA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI
More Speeches
images Ask the Director of Elections

R.R. Kiravu - Director of Elections

R.R. Kiravu
Director of Elections
images Documents and Publications
images WebMail Login
images
Click to read Mail
(Staff only)
images Photo Gallery

images
More Photos

images Calendar of Events
 <<  < Sep 2010 >   >>
SMTWThFS
1234
56789
10
11
12131415161718
19202122232425
2627282930